• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Super Eagles ya Nigeria yapiga Benin na kufuzu kwa fainali za AFCON 2022

Super Eagles ya Nigeria yapiga Benin na kufuzu kwa fainali za AFCON 2022

Na MASHIRIKA

NIGERIA walifuzu kwa fainali za Kombe la Afrika (AFCON) 2022 baada ya kuwapiga Benin 1-0 katika Kundi L mnamo Jumamosi mjini Porto Novo.

Bao la pekee na la ushindi katika mechi hiyo lilipachikwa wavuni na Paul Onuachu katika dakika ya 93.

Katika mechi nyingine ya Kundi hilo, Lesotho waliambulia sare tasa na Sierra Leone.

Matokeo hayo yanamaanisha kwamba Sierra Leone kwa sasa wana ulazima wa kushinda Benin katika mchuano utakaowakutanisha jijini Freetown mnamo Machi 30 ili kufikia idadi sawa ya alama na Benin.

Ikitokea hivyo, Sierra Leone watajikatia tiketi ya kuelekea Cameroon kwa minajili ya fainali za 2022 kwa wingi wa mabao.

Super Eagles ya Nigeria bado itamaliza kampeni za Kundi L kileleni hata iwapo watapigwa na Lesotho katika mechi yao ya mwisho mnamo Machi 30, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Ivory Coast na Morocco wajikatia tiketi za kushiriki...

Luxembourg wazamisha chombo cha Jamhuri ya Ireland