• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Uswidi wapepeta Armenia 3-1 kirafiki

Uswidi wapepeta Armenia 3-1 kirafiki

Na MASHIRIKA

BEKI matata wa Manchester United, Victor Lindelof aliwasaidia Uswidi kukomoa Armenia 3-1 katika mchuano wao wa mwisho wa kujiandaa kwa fainali za Euro.

Baada ya wenyeji Uswidi kuwekwa kifua mbele na Emil Forsberg na Marcus Danielson katika dakika za 16 na 34 mtawalia jijini Stockholm, kiungo wa zamani wa Arsenal na Birmingham City, Sebastian Larsson alishuhudia mkwaju wake wa penalti kupanguliwa na kipa wa Armenia.

Lindelof pia alipoteza mkwaju wa penalti kabla ya Vahan Bichakhchyan kuwarejesha Armenia mchezoni. Hata hivyo, Marcus Berg alitokea benchi na kuwarejeshea Uswidi uongozi wa mabao mawili.

Uswidi wameratibiwa kuanza kampeni zao za Euro 2020 dhidi ya Uhispania mnamo Juni 14 jijini Seville.

Baada ya hapo, miamba hao walioambulia nusu-fainali za Euro mnamo 1992, wataelekea St Petersburg kuvaana na Slovakia mnamo Juni 18 kabla ya kupimana ubabe na Poland siku tano baadaye.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Carlos Tevez kujiengua kambini mwa Boca Juniors ya...

Wanavyuo kupokea ufadhili wa wa Sh4.5 milioni kutoka kwa...