NA JAMES MURIMI
KATIBU Mkuu wa chama cha Jubilee, Bw Jeremiah Kioni amesema hatajali hata kama atakuwa kiongozi wa pekee kubaki katika chama hicho huku migawanyiko ikiendelea kudhihirika.
Baadhi ya wabunge wa chama hicho wametangaza kushirikiana na serikali ya Rais William Ruto huku Bw Kioni akionekana kubaki peke yake kuendeleza ajenda za Jubilee katika muungano wa upinzani wa Azimio la Umoja One Kenya.
Bw Kioni alisema chama hicho kina wanachama wengi kote nchinini na hakitalemazwa na viongozi wachache wanaojiunga na serikali ya Kenya Kwanza.