• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 8:50 PM
Ruto apiga kura katika kituo cha Kosachei

Ruto apiga kura katika kituo cha Kosachei

NA ONYANGO K’ONYANGO

NAIBU Rais Dkt William Ruto amepiga kura saa kumi na mbili asubuhi katika kituo cha kura kilichoko katika Shule ya Msingi ya Kosachei eneobunge la Turbo, Kaunti ya Uasin Gishu.

Dkt Ruto anayewania urais kwa tikiti ya United Democratic Alliance (UDA) aliyefika kituoni akiwa na mkewe Rachel Ruto muda wa dadika mbili kabla kituo kufunguliwa rasmi amesema aliamua kuwahi mapema ili kuepusha hali ya kuwachelewesha wapigakura wengine kutekeleza haki yao ya kidemokrasia.likuwasaid because of his stature, and political clout he felt voting during the day would become an unnecessary inconvenience to those who would be in the lines.

“Kila mpigakura hapa anataka uchaguzi wa amani. Maombi yetu kabla ya uchaguzi huu yalikuwa ni tuwe na uchaguzi wa amani. Nina furaha kwamba uchaguzi huu unatoa fursa ya kipekee ya enzi mpya ya utawala nchini,” amesema.

  • Tags

You can share this post!

Kafyu yasitishwa Marsabit, Kerio kuwezesha kura

Mahakama ya Juu yatesa wabunge kwa kuzima CDF

T L