• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:50 AM
Ruto ashindwa kupatanisha wandani wake wanaong’ang’ania ugavana Kajiado

Ruto ashindwa kupatanisha wandani wake wanaong’ang’ania ugavana Kajiado

NA STANLEY NGOTHO

NAIBU Rais William Ruto anaonekana kushindwa kuwapatanisha wawaniaji ugavana wa Kajiado Mbunge wa Kajiado Mashariki Peris Tobiko na mwenzake wa Kajiado Kusini Katoo Ole Metito.

Wawili hao ambao ni wandani wake wamekataa kupatana na wameamua kukabiliana katika kura ya mchujo mnamo Aprili 14.

Aliyekuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani (NTSA) Francis Meja pia anashindania tikiti ya chama cha United Democratic Alliance (UDA).

Juhudi za kiongozi wa UDA Naibu Rais William Ruto, za kupatanisha wawaniaji hao watatu ili wawili waweze kumuunga mkono mmoja wao.

Wawaniaji hao wamekuwa wakiendesha kampeni zao katika maeneo mbalimbali ya kaunti ya Kajiado kujipigia debe.

Dkt Ruto amechelea kuzuru kaunti hiyo ili asionekane kana kwamba anaunga mkono mgombeaji fulani.

Katika wiki mbili zilizopita, wawaniaji hao wameonekana wakiendesha kampeni katika maeneo ya vijiji wanakoishi watu wa asili ya Maasai.

Awali, wanasiasa hao waliendesha kamp – eni kali katika maeneo ya miji kama vile Ngong’, Ongata Rongai, Kiserian na Kitengela.

Miji hiyo inayokaribiana na jiji la Nairobi, ina asilimia 60 ya idadi jumla ya wapiga kura katika kaunti ya Kajiado.

Kufikia sasa wawaniaji hao watatu wamechelea kutaja majina ya wagombeaji wenza wao.

  • Tags

You can share this post!

Pasaka: Hoteli zafurika

Turuhusiwe kuagiza mahindi kutoka nje – Kampuni za...

T L