• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
UDA kufanya uchaguzi wa mashinani Oktoba – Muthama

UDA kufanya uchaguzi wa mashinani Oktoba – Muthama

 

Na ONYANGO K’ONYANGO

CHAMA cha United Democratic Alliance (UDA), kinachohushwa na Naibu Rais William Ruto, kitafanya uchaguzi wa mashinani Oktoba mwaka huu, kabla ya mchujo wa wawaniaji wake kwenye uchaguzi mkuu wa 2022.

Uchaguzi huo ulikuwa umepangwa kufanyika Juni 18 lakini ukaahirishwa. Washirika wa Dkt Ruto wamekuwa wakipigia debe chama hicho wakisema, ndicho atatumia kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu ujao naada ya kutofautiana na Rais Kenyatta.

Wanasema chama kitaandaa uchaguzi wa mashinani kabla ya kuteua wawaniaji hili kuepuka makosa yaliyofanywa na Jubilee.

Kulingana na mwenyekiti wa UDA, Johnstone Muthama, ili mwanachama aruhusiwe kushiriki uteuzi wa chama, ni lazima awe mwanachama, kumaanisha kama vyama vingine, kitahitajika kuwa na orodha ya wanachama

.Bw Muthama anasema hatua hiyo itakipatia chama hicho nguvu kuliko vyama pinzani ambavyo huteua watu kuwa kaimu maafisa.

 

You can share this post!

JAMVI: Kalonzo alivyowazidimaarifa magavana wa Ukambani

Wazee wa Kaya sasa wavuruga karata za Jumwa