• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Washirika wa Ruto wapuuza chama kipya cha Lonyangapuo

Washirika wa Ruto wapuuza chama kipya cha Lonyangapuo

Na OSCAR KAKAI

WASHIRIKA wa Naibu wa Rais William Ruto Kaskazini mwa Bonde la Ufa, wamepuuzilia mbali chama kipya cha Kenya Union Party (KUP) kinachoongozwa na Gavana wa Kaunti ya Pokot Magharibi John Lonyangapuo na mbunge wa Pokot Kusini David Pkosing wakisema hakitaleta mabadiliko yoyote eneo hilo.

Viongozi hao wanataka kutumia chama hicho kipya kutetea viti vyao kwenye uchaguzi mkuu ujao suala ambalo huenda likaathiri umaarufu wa vyama vya Kanu, Jubilee na UDA.

Wandani wa Naibu wa Rais wameanzisha mchakato wa kukipigia debe chama cha United Democratic Alliance (UDA).

Wakiongea na wanahabari mjini Kapenguria, washirika wa Dkt Ruto wakiongozwa na mbunge wa Kacheliba Bw Mark Lomunokol, wanasema KUP hakina umaarufu.

You can share this post!

Mwenye mazoea ya kuibia wenye maduka ya Mpesa achapwa kama...

KDF kusaidia kukabiliana na ukame