• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
WACHIRA ELISHAPAN: Matatizo yatakayoikumba IEBC ni mwiba wa kujichoma

WACHIRA ELISHAPAN: Matatizo yatakayoikumba IEBC ni mwiba wa kujichoma

NA WACHIRA ELISHAPAN

Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya (IEBC) bila shaka inafanya kazi yake itakikanavyo bila kuwa na msukumo wowote kutoka kwa wadau mbalimbali nchini. Hatua hii kwa hakika inadhihirisha kuwa tume hiyo kuwa huru na isiyopendelea upande wowote wa kisiasa wala wa kidini.

Huenda matatizo yanayoiandama tume hii kwa sasa ni mwiba wa kujichoma usioabiwa pole. Masaibu ya tume hii yalianza tangu mwaka wa 2017 ambapo tume hii iliandaa uchaguzi ambao kulingana nao ulikuwa huru.

Uchaguzi huo ulijawa na siasa zisizo na kipimo na baada ya baadhi ya mwaniaji mmoja kukimbilia mahakamani, jaji mkuu Jaji David Maraga baada ya kusikiliza na kukagua ushahidi uliotolewa ,ikabainika wazi kuwa kulikuwa na mushikli katika uchaguzi huo.

Ilibainika wazi kwamba uchaguzi huo haukupangwa kwa njia inayofaa na kwa hivyo malalamishi yote yakaelekezwa kwayo. Tangu hapo Wafula Chebukati amekuwa akionekana kama mtu asiyetaka mazuri kwa serikali.

Uchaguzi wa urais uliporudiwa,na Rais Uhuru Kenyatta kuibuka mshindi pamoja na naibu wake William Ruto,tume hiyo ilionekana kama isiyoutakia mazuri mrengo wa kiongozi wa ODM Raila Odinga na tangu hapo,huenda ndipo uhasama ulitokea baina yao.

Mara tu Raila Odinga waliposalimiana katika salamu za heri njema na rais Uhuru Kenyatta,huenda ndipo mambo yaliigeuka tume hiyo inayoongozwa na Wafula Chebukati.

Tangu uchaguzi huo uliokuwa na utata,kiongozi wa ODM Raila Odinga hajakuwa na imani na tume hiyo na anaitaka kubanduliwa kisha ikaundwa upya ikiwa na makamishna wapya. Hoja ya kuunda ripoti ya jopo la maridhiano la BBI ilipobuniwa,Odinga hakuwa budi kuweka wazi azimio lake la kuibandua tume hiyo.

Hatua ya kwanza ambayo IEBC ilionekana kuchukua baada ya saini za BBI kupokelewa,ilikuwa ni kuitisha fedha za shughuli hizo zote bila hata ya kubaini kwamba itachukua muda gani.

Mzozo kati ya IEBC na Raila Odinga ukatokota upya, tume hiyo ilipodai kima kikubwa cha pesa huku naye Odinga akikisia kiasi cha dola moja kwa kila mpiga kura katika kupiga kura ya maamuzi.

Hatua hii bila shaka huenda ikawa inaonyesha wazi msimamo wa IEBC jambo ambalo halifai kwa tume huru, na tayari tume hiyo imeanza kukagua sahihi hizo japo sasa haijulikani jinsi hali ilivyo katika kambi ya Odinga.

Kenya ina historia ya kubandua tume za uchaguzi kila baada ya uchaguzi,jambo ambalo huibua maswali kuhusu jinsi mfumo wa uongozi unavyotekelezwa.

Mara tu baada ya uongozi wa rais mstaafu Mwai KIbaki kuondoka, tume iliyokuwepo ya ECK ilibanduliwa kasha baadaye ikaundwa tume ya muda ya IIEC na baadaye IEBC tume ambayo inachelea kubanduliwa iwapo mapendekezo ya ripoti ya maridhiano ya BBI yatapitishwa na kuwa sheria.

You can share this post!

Kibarua kigumu kwa wanavoliboli wa Kenya kimataifa

Dhana na dhima ya malipo mbalimbali katika jamii