• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Nyong’o apigwa kumbo na wandani wake wa zamani

Nyong’o apigwa kumbo na wandani wake wa zamani

Na Rushdie Oudia

GAVANA wa Kisumu, Prof Anyang’ Nyong’o, anakabiliwa na pingamizi kubwa kuhusu azimio la kuwania wadhifa huo kwa mara ya pili mwaka wa 2022.

Wandani wake wengi waliomuunga mkono wakati wa uchaguzi uliopita sasa wameungana kutaka mmoja wao amtimue.

Wanajumuisha Seneta Fred Outa, Mbunge Mwakilishi wa Wanawake Rozah Buyu, aliyekuwa mkuu wa wafanyakazi katika Kaunti ya Kisumu Patrick Ouya Kalausi ambao kwa pamoja waliunda kikosi cha ‘Team Kali’ kumng’oa mamlakani aliyekuwa gavana Jack Ranguma.

“Tutaungana na kujulisha kaunti na taifa zima kuhusu jinsi gavana ameshindwa kutimiza ahadi zake,” akasema Bw Outa.

Hata hivyo, Bw John Oywa ambaye ni msemaji wa Prof Nyong’o alisema gavana kwa sasa anajishughulisha na maendeleo kwa hivyo hatajibizana na mahasimu wake wa kisiasa.

“Gavana ni baba wa kaunti hii na hana haja kujibizana na wakosoaji wake kwa masuala yasiyo na msingi,” akajibu Bw Oywa.

 

You can share this post!

Nyota wa ‘Vuta Pumzi’ alifariki kutokana na...

Hofu uvamizi wa nzige unapunguza asali