• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
Kaunti ya Nyeri yalenga kuchanja wanabodaboda 2,000

Kaunti ya Nyeri yalenga kuchanja wanabodaboda 2,000

Na SAMMY WAWERU

KAUNTI ya Nyeri inalenga kuwapa wahudumu wapatao 2, 000 wa afya chanjo ya Homa ya virusi vya Corona. Gavana wa Kaunti hiyo, Bw Mutahi Kahiga amesema shughuli ya utoaji wa chanjo hiyo aina ya AstraZeneca tayari imeanza.

“Nyeri inalenga kuchanja wahudumu 2, 000 wa afya,” akasema Bw Kahiga.

Licha ya hofu kuibuka miongoni mwa Wakenya kuhusu usalama wa chanjo inayotolewa, Gavana Kahiga alisema watakaopokea Nyeri itakuwa kwa hiari.

“Utoaji wa chanjo ni kwa hiari, hakuna atakayelazimishwa. Hata hivyo, ninahimiza wahudumu wa afya wajikinge,” akasema.

Bara Uropa imesimamisha utoaji wa chanjo ya AstraZeneca, kufuatia visa kadha vya maafa ya wahudumu wa afya, baada ya kuchanjwa.

Nchi za Bara Ulaya zilizosimamisha utoaji wa chanjo hiyo ni pamoja na Norway, Denmark, Iceland, Bulgaria, Ireland, Netherlands, France, Italy na Germany.

Denmark na Norway wameandikisha visa kadha vya maafa baada ya wahudumu wa afya kuchanjwa.

Rais Uhuru Kenyatta hata hivyo amewahakikishia Wakenya kwamba wahudumu wa afya wako macho kushughulikia hali zozote ambazo huenda zikatokea, baada ya kupata chanjo.

Gavana Kahiga alisema baada ya wahudumu wa afya Nyeri kupata chanjo, serikali yake itaelekea kwa walimu na maafisa wa usalama kaunti hiyo.

Nyeri imeandikisha zaidi ya visa 1, 300 vya maambukizi ya Covid-19, huku 50 wakiripotiwa kuangamizwa na ugonjwa huo.

You can share this post!

Hit Squad kuelekea Congo Ijumaa

Manyota FC na Fafada kukutana fainali ya Sebe Legends Cup