• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
FAUSTINE NGILA: Heko AU kuunda teknolojia ya paspoti za kidijitali

FAUSTINE NGILA: Heko AU kuunda teknolojia ya paspoti za kidijitali

NA FAUSTINE NGILA

Je, unafahamu kuwa safari zote za ndege sasa zinawalazimu wasafiri kuwa na paspoti ya corona kando na ile ya kawaida? Mataifa yaliyoendelea yalikuwa ya kwanza kuleta mfumo huu lakini sasa bara la  Afrika limekumbatia teknolojia mpya ya paspoti za kidijitali.

Ni mtindo ambao utandelea kutumika katika viwanja vya ndege kote duniani, hata iwapo maambuziki mapya ya corona yatapyngua.

Kwa hili, mataifa ya Afrika, licha ya kukosekana kabisa katika juhudi za kuunda chanjo ya corona, raundi hii yamekuwa miongoni mwa mataifa ya kwanza kuunda paspiti ya kidijitali kwa kutumia teknolojia yake yenyewe.

Kampuni za ndege za Afrika tayari zimeanza kukumbatia teknolojia hiyo iliyoundwa na Umoja wa Afrika (AU) kurahisisha usafiri, katika kipindi ambapo usafiri wa ndege umelemazwa na ukosefu wa vipimo na vyeti vya corona.

Kampuni za Kenya Airways na Ethiopian Airlines zimeungana na Shirikisho la Usafiri wa Angani Afrika Magharibi na Kati (ASKY) kutumia mfumo wa kidijitali wa PANABios unaoendeshwa na AU ikishirikiana na Vituo vya Kuzuia Magonjwa Afrika (Africa CDC).

Jukwaa hilo la kidijitali kwa jina Trusted Travel Pass litawezesha abiria kuthibitisha vipimo vyao na vyeti vya corona kwa haraka kabla ya kupanda ndege, ithibati kuwa Afrika sasa imekomaa kiteknolojia na inaweza kujitegemea.

Ingawa teknolojia za mabara mengine bado zipo, AU imeonekana kuwa mstari wa mbele kuhamasisha mataifa yote kutumia teknolojia hiyo kama njia moja ya kusaidia kampuni za ndege brani kuongoza mapato katika kipindi hiki kigumu cha biashara.

Wateja sasa wanafurahia safari za angani bila bughudha wakitumia paspoti za kidijitali, kwani zimewawezesha maafisa katika viwanja vya ndege kutambua iwapo abiria wamechanjwa na kama wametimiza masharti ya kudhibiti virusi vya corona.

Binafsi nimependezwa na juhudi za AU kwa kuhakikisha bara la Afrika lina mtandao wake wa kuthibitisha vipimo vya corona kupitia kwa maabara, hali ambayo inahakikisha biashara inaendelea kama kawaida miongoni mwa mataifa ya Afrika.

Kwa mara ya kwanza, Waafrika tumeungana kukataa teknolojia za majuu ambazo gharama yake iko juu, na kujikubali kwamba tuna ubunifu wa kutosha kuoambana na changamoto ztu wenyewe.

Hata hivyo, baadhi ya mataifa bado yanazembea kuchangamkia jukwaa hilo, hata wakati yanajua fika kuwa vyeti vya corona vya kidijitali vinahitajika iwapo taifa linafanya biashara ya uchukuzi wa angani.

Mataifa hayo yanapaswa kukoma kutilia shaka juhudi za AU, kwani teknolojia yake imeundwa kwa kiwango cha kimataifa kuwajali Waafrika wote bila ubaguzi na kutokomeza ufisadi katika sekta ya afya, huku ikipunguza gharama ya vipimo vya maabara.

Cha muhimu ni kuwa huu ni mfumo ambao utatusaidi kukusanya data yetu binafsi kutuwezesha kufanya maamuzi ya kibiashara haraka, kando na mazoea ya mabara mengine ya kukama data katika uchumi wa Afrika bila hata kulipia senti.

Iwapo mfumo huo wa PANABios  utatumiwa na mataifa yote, utaboresha usimamizi wa sera kote Afrika na kuinua biashara baina ya mataifa, kupiga jeki utalii, uwekezaji na utamaduni, na hatimaye kuhakikisha Afrika haiachwi nyuma na mabara mengine katika maendeleo.

 

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Majangili wenye silaha kali wazidi...

WASONGA: Mvutano wa Kenya, Uingereza kuhusu Covid haustahili