Na MASHIRIKA
N’DJAMENA, CHAD
JESHI nchini Chad limetangaza Jumanne kwamba Rais Idriss Deby Itno aliyeibuka mshindi wa uchaguzi wa Urais, Aprili 11, 2021, akitafuta awamu ya sita Deby Itno, amefariki akiwa mstari wa mbele wa makabiliano baina ya wanajeshi na kundi la waasi.
Taarifa ya msemaji wa jeshi Jenerali Azem Bermandoa Agouna imesema alifariki akipigania usalama wa taifa hilo ambalo ameliongoza kwa muda wa miaka 30.
Deby amekumbana na kifo akiwa na umri wa miaka 68.
Kwa mujibu wa jeshi, baraza la kijeshi linaloongozwa na mwanawe ambaye ni Mahamat Idriss Deby Itno, 37, linasimamia nchi hiyo kipindi hicho cha msiba.