• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Mshukiwa mkuu wa mauaji ya afisa wa NLC anyakwa

Mshukiwa mkuu wa mauaji ya afisa wa NLC anyakwa

Na CECIL ODONGO

IDARA ya Upelelezi Nchini (DCI) imesema kwamba imemtambua na kumkamata mshukiwa mkuu katika mauaji ya afisa wa Tume ya Kitaifa ya Ardhi (NLC), Bi Jennifer Wambua aliyeuawa Aprili.

Kulingana na taarifa kwenye ukurasa wake wa Twitter, DCI ilisema uchunguzi wao ulibaini kuwa Bw Peter Mwangi Njenga kwa jina la utani Ole Sankale alionekana na marehemu siku ya mwisho Machi 12, 2021.

Mwangi alikamatwa Aprili na makachero wa DCI nyumbani kwake Embulbul, Ngong’, Kaunti ya Kajiado. Embulbul ni karibu na mahali ambapo mwili wa Bi Wambua ulipatikana katika kichaka cha wazi eneo la Kerarapon.

“Kutokana na uchunguzi uliohusisha utaalamu wa hali ya juu, makachero wamebaini kuwa mshukiwa alitangamana na marehemu na kuwa naye katika eneo ambalo mwili wake ulipatikana,” ikasema DCI.

Mwangi alimfuata Bi Wambua hadi msitu wa Ngong alikoelekea ili kuomba kabla ya mwili wake kupatikana akiwa nusu uchi na uchunguzi wa DCI ulithibitisha kuwa alikuwa eneo la mauaji.

  • Tags

You can share this post!

Mashambulio yatokea Afghanistan kipindi Amerika iko mbioni...

CHOCHEO: Asali sio leseni ya ndoa