• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Gozi la Community Shield kati ya Man-City na Leicester kutandazwa Agosti 7 ugani Wembley

Gozi la Community Shield kati ya Man-City na Leicester kutandazwa Agosti 7 ugani Wembley

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

KIPUTE cha kuwania taji la Community Shield kati ya Manchester City ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na Leicester City ambao ni wafalme wa Kombe la FA sasa kitachezewa uwanjani Wembley, Uingereza mnamo Agosti 7, 2021.

Idadi ya mashabiki watakaohudhuria mchuano huo itafichuliwa na waandalizi katika wiki zijazo na itategemea jinsi ambavyo janga la corona litakuwa limedhibitiwa nchini Uingereza.

Man-City wanajivunia taji la Community Shield mara sita huku Leicester wakijitwalia kombe hilo mara moja pekee mnamo 1971. Kivumbi cha Community Shield huashiria mwanzo wa kampeni za EPL.

Kampeni za EPL kwa ajili ya msimu wa 2021-22 zimeratibiwa kuanza katika wikendi ya Agosti 14 na 15, 2021.

You can share this post!

Phil Foden wa Man-City ndiye mwanasoka mwenye thamani ya...

Amerika yapepeta Mexico kwenye fainali ya Concacaf Nations...