Na MASHIRIKA
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO
KIPUTE cha kuwania taji la Community Shield kati ya Manchester City ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na Leicester City ambao ni wafalme wa Kombe la FA sasa kitachezewa uwanjani Wembley, Uingereza mnamo Agosti 7, 2021.
Idadi ya mashabiki watakaohudhuria mchuano huo itafichuliwa na waandalizi katika wiki zijazo na itategemea jinsi ambavyo janga la corona litakuwa limedhibitiwa nchini Uingereza.
Man-City wanajivunia taji la Community Shield mara sita huku Leicester wakijitwalia kombe hilo mara moja pekee mnamo 1971. Kivumbi cha Community Shield huashiria mwanzo wa kampeni za EPL.
Kampeni za EPL kwa ajili ya msimu wa 2021-22 zimeratibiwa kuanza katika wikendi ya Agosti 14 na 15, 2021.