• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Wanachama 500 wagura UDA na kurejea ODM

Wanachama 500 wagura UDA na kurejea ODM

KNA na CHARLES WASONGA

ZAIDI ya wanachama 500 wa chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika eneobunge la Karachuonyo wamehamia chama cha ODM kwa madai ya kutelekezwa na chama hicho kinachohusishwa na Naibu Rais William Ruto.

Wanachama hao wanadai kuwa chama hicho kinajihusisha zaidi na shughuli za kutengeneza pesa na kufumbia macho matakwa yao.

Akiongea na KNA, aliyekuwa mshirikishi wa UDA eneobunge la Rachuonyo Duncan Ombat alisema chama hicho kimekuwa kikiendeleza usajili wa wanachama wapya eneo hilo kisiri bila kuwahusisha.

Bw Ombat alisema wanachama waliogura chama hicho walifanya hivyo kwa sababu hawakutaka kuhusishwa na shughuli hiyo haramu na iliyolenga kuwahadaa.

“Hakukuwa na demokrasia ndani ya ODM katika shughuli za mchujo kuelekea uchaguzi mkuu uliopita na ndiposa tukahama na kujiunga na UDA. Tulitarajia kuwa matakwa yetu yangeshughulikiwa katika chama hiki kipya lakini hili halijatendeka,” akasema Ombat.

Aliyekuwa mwenyekiti wa UDA katika eneobunge hilo Jekonia Olango aliunga mkono kauli hiyo akisema wamekuwa wakikumbwa na changamoto mbalimbali kuendesha afisi za tawi la UDA katika eneo hilo.

You can share this post!

Usimpake tope Raila, wabunge wa ODM wamuonya Ruto

CECIL ODONGO: Matamshi ya Raila kikwazo kwa azma yake kuwa...