• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Wabunge watisha kumtimua Magoha

Wabunge watisha kumtimua Magoha

Na Florah Koech

WABUNGE watatu kutoka Kaunti ya Baringo, wametishia kuwasilisha hoja ya kumtimua Waziri wa Elimu Profesa George Magoha kutokana na kile walichosema ni kutoa amri zinazovuruga utendakazi wa wizara yake.

Mbunge wa Baringo Kusini Charles Kamuren, Daniel Tuitoek (Mogotio) na Joshua Kandie wa Baringo ya Kati walisema kwamba sekta ya elimu iko katika hatari ya kuporomoka kabisa kutokana na amri na sera za Profesa Magoha ambazo waziri huyo hukumbatia bila kushauriana na wadau wengine.

Wanasiasa hao hasa walisikitishwa na amri ya Profesa Magoha kuwa mabasi ya shule hayafai kutumiwa kwenye hafla za kibinafsi na shughuli za kijamii.

Pia walishutumu amri yake kwamba shule ambazo hazina watahiniwa zaidi ya 40 wa KCPE na KCSE ziunganishwe pamoja na hitaji la walimu wa shule za msingi kuwa na cheti cha Diploma.

“Hatuna taasisi yoyote ya kutoa mafunzo ya ualimu hapa Baringo ya Kati. Pia si wanafunzi wengi kutoka hapa ambaye waliofuzu vyema na kuhitimu kujiunga na taasisi hizo. Amri ya Profesa Magoha kuhusu elimu inakera na inabagua jamii zilizotengwa,” akasema Bw Kandie.

Kusomea ualimu, Wizara ya Elimu imesema kwamba wanafunzi lazima wawe na alama ya C wastani katika KCSE na alama sawa na hiyo katika lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

“Iwapo Profesa Magoha hatabadili mtindo wake wa uongozi na kuondoa amri hizo alizoziweka, basi niko tayari kuwasilisha hoja ya kumtimua bungeni,” akaongeza Bw Kandie.

You can share this post!

Mizozo ya wanasiasa yaua ziara ya Uhuru Ukambani

Matiang’i aahidi kukomesha utekaji nyara nchini