• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Polo ajifanya sonko kumbe kijijini ni hoi

Polo ajifanya sonko kumbe kijijini ni hoi

YALA, Siaya

Na JOHN MUTUKU SAMUEL

KALAMENI eneo hili alibubujikwa na machozi na kujitupa miguuni mwa demu kumuomba asimteme lakini hilo halikusaidia kitu.

Jamaa alikuwa amempeleka demu kwao lakini akagundua hakuwa na mbele wala nyuma licha ya kuishi maisha ya kujishasha mjini.“Nimeamua kukuacha kwa kuwa nilidhania wewe ni dume kumbe hata wanawake wamekushinda kwa maendeleo,” mchumba alimsimanga mbele ya watu.

“Mwanamume wa kisasa ni maendeleo si ukubwa wa misuli na kifua kipana. Nilitarajia kuona maendeleo hapa nyumbani lakini huna lolote la kuringia. Usiwahi kunisumbua ukinipigia simu,” demu alisema, akampungia mkono na kuondoka.

Jamaa na mchumba wake waliishi mjini. Demu alimpenda mwanamume huyo kutokana na maisha ya ‘high class’ aliyoishi. Aliishi nyumba kubwa, iliyokuwa na redio ya kisasa, runinga kubwa, friji, maikrowevu, makochi, makabati na zulia la thamani.

Jombi alikuwa mtu wa majivuno, demu akaamini huyo alitoka katika familia tajiri sana hadi juzi alipompeleka nyumbani kwao.Demu alishangaa kwa kuwa jombi alikuwa na nyumba ndogo ya chumba kimoja yenye mlango wa bati na paa la nyasi.

Kwa kuwa ulikuwa ni usiku, demu alivumilia kunguni na chawa usiku kucha waliomtafuna kwelikweli.“Wapo wanaume duniani ila wewe si mmoja wao. Bado una utoto mwingi kichwani ndio maana wanaume wa rika lako wakisonga mbele, nawe unarudi nyuma,” demu alimwambia.

Juhudi za jombi kumrai demu amvumilie hazikuzaa matunda. Demu alikuwa amegundua kwamba, hata angalikubali kuolewa na jamaa, angekabiliana na maisha magumu yenye dhiki ndio maana akaamua kumtema harakaharaka.

“Umeachwa kwa kupenda raha ya mji badala ya kukumbuka kwamba maisha ya mji hufikia mwisho mtu akakumbuka kurejea nyumbani,” jombi alisutwa na kaka yake.

You can share this post!

Wahudumu wa baharini watakiwa kuzingatia sheria

Mwanamume aliyedaiwa kujifanya hakimu ashtakiwa

T L