• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Polo auguza nyeti kisiri nyumbani

Polo auguza nyeti kisiri nyumbani

Na JOHN MUTUKU SAMUEL

PIPELINE, NAIROBI

POLO mtaani hapa alijifungia ndani ya nyumba kwa siku kadhaa kujiuguza baada ya kufinywa sehemu nyeti na kidosho aliyejaribu kumpapasa wakiwa kwenye matatu.

Jamaa aligundua kwamba, si wanawake wote wa kudhalilishwa.Kulingana na mdokezi, polo alikuwa na mazoea ya kutongoza na kudhalilisha wanawake wa kila sampuli.

Alifanya mambo hayo hadi akawa mzoefu, woga ukamuondoka, akawa tayari kuwatesa wanawake.

Siku ya tukio, polo alisimama steji kusubiri demu mmoja aliyevalia sketi fupi alipowasili.

“Hili totoshoo siliachi, wallahi billahi siliachi. Lazima nilitongoze litake lisitake,” polo aliambia makanga.

Polo alihakikisha kwamba aliketi kiti kimoja na demu huyo. Baada ya salamu alianza kurusha mistari.

“Vipi dada, wapendeza mno,” polo alisifia.

“Shukran ila kaka mie ni mke wa mtu. Nishapita kiwango cha kutongozwa,” demu alitoa msimamo.

“Siku hizi uwe umeoa au umeolewa, kutongozana ni kawaida dada,” polo alijibu.

“Utongoze nani? Jipe shughuli mhuni wewe,” dada alikuja juu.

Ghafla taa garini ilizimika.

Polo alichukua fursa hiyo kunyoosha mkono kuelekea kwenye kifua cha dada.

Kisura aliudaka ule mkono, akazamisha kucha zake kali kisha akamkamata nyeti zake na kuanza kuzifinya kisawasawa.

Polo alijaribu kupiga nduru za kuomba msaada akashindwa. Alifuta jasho na kamasi jingi likamtoka.

“Utarudia kuwatongoza wengine?” demu alimnong’onezea.

Polo aliishia kujibu kwa ishara kwamba asingerudia.

“Najua steji unayoshukia. Shuka na usitazame nyuma,” demu alimshauri.

Polo alipoachiliwa, alichechemea kwa tabu hadi akashuka garini. Hakutazama nyuma. Alielekea nyumbani kujiuguza majeraha.

“Huyo sio wale wanawake ambao nimekuwa nikidhalilisha,” jamaa alijiambia kimoyomoyo.

You can share this post!

Waiguru adai ni vigumu kuchaguliwa kupitia Jubilee

‘Ruto alishika Uhuru mateka’