• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:50 AM
Afisa aliyeangamiza mtoto Juni 12, 2022 hajaadhibiwa mwaka mmoja baadaye

Afisa aliyeangamiza mtoto Juni 12, 2022 hajaadhibiwa mwaka mmoja baadaye

NA MERCY KOSKEI

AFISA mmoja mkuu wa polisi anayehusishwa na mauaji ya Whitney Atieno, mwanafunzi wa shule ya upili, katika mtaa wa Lake View Nakuru ameachiliwa huru mwaka mmoja baada ya kisa hicho kilichowakera wakazi.

Inadaiwa kuwa Atieno, 19 ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Upili ya Nakuru Central, alipigwa risasi na afisa huyo.

Wakati huo, Juni 12, 2022, polisi huyo alikuwa akihudumu kama Afisa Msimamizi wa Kituo cha Polisi (OCS), na alikuwa akiongoza operesheni ya kuwanasa wanachama wa genge la wahalifu kwa jina “confirm”.

Inasemekana kuwa ushahidi wa kumhusisha afisa huyo, jina limebanwa, ‘moja kwa moja na mauaji ya mwanafunzi huyo.’

 

  • Tags

You can share this post!

Dereva: Rais Ruto aendesha gari linalotumia nguvu za umeme...

Nyani wasumbufu wanaovamia kuku na kutwanga walevi barabara...

T L