• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Aliniacha akaolewa, sasa anataka tuoane baada ya kuachana na mume wake

Aliniacha akaolewa, sasa anataka tuoane baada ya kuachana na mume wake

SHANGAZI;

Mpenzi tuliyeachana amerudi kwangu akiomba turudiane. Aliniacha miaka miwili iliyopita akaolewa na mtu mwingine na sasa wameachana. Naomba unishauri wako.

Unafaa kujiuliza ni kitu gani kimewafanya wawili hao kuachana muda mfupi tu baada ya kufunga ndoa. Huenda ndiye mwenye shida na ndiyo sababu ametemwa. Usikubali kuvunjwa moyo tena.

Mke wangu amefutwa na bosi aliyemtorosha

Nilimwacha mke wangu nilipogundua alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na bosi wake kazini. Miezi miwili iliyopita waliachana na akafutwa kazi. Sasa anatumia mtoto wetu kunipigia simu akiomba turudiane. Nifanyeje?

Hatua yake ya kutumia mtoto ni kuvuta hisia na huruma zako. Kama humtaki, badilisha namba yako ya simu ili aache kukusumbua. Mtoto akiwa mtu mzima ataamua iwapo ataishi na mama yake au atarudi kwako.

Nimesikia alikuwa na mke na wakaachana kabla ya kunioa

Nimepata habari kwamba mpenzi wangu alikuwa ameoa lakini akaachana na mke wake miaka miwili iliyopita. Nimemuuliza kuhusu habari hizo na amekana. Nifanye nini?

Utakosea kuchukua hatua kwa kutegemea habari za kuambiwa. Zinaweza kuwa za kweli ama za uongo. Ni muhimu uchunguze kwanza ujue ukweli wake ndipo upate mwelekeo kuhusu uhusiano wenu.

Alikuwa akinipigia simu kila siku, siku hizi mwezi unaisha bila kumsikia

Mwanamume mpenzi wangu alikuwa akinijulia hali karibu kila siku na pia tulikutana kila wikendi. Siku hizi anamaliza hata wiki bila kunipigia simu. Mwezi mzima sijamuona, anadai amekosa nafasi.

Mtu anayekupenda hawezi kumaliza wiki nzima bila kukujulia hali. Inawezekana kwamba ameamua kuvunja uhusiano wenu lakini anashindwa kukwambia. Ondoa mawazo yako kwake

  • Tags

You can share this post!

Korti yamwacha Mackenzie kwa mataa

‘Wakili feki’ Brian Mwenda kusherehekea...

T L