• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Dereva ashtakiwa kuteka nyara polisi

Dereva ashtakiwa kuteka nyara polisi

NA RICHARD MUNGUTI

DEREVA wa gari la kibinafsi na abiria wake Jumanne walishtakiwa kumteka nyara afisa wa polisi.

Afisa huyo Koplo Nickson Sambach, mahakama ilieleza, alitekwa nyara na Cosmus Kaai Kinyua na Wyclife Nyagena Ogare mnamo Machi 17, 2022 katika eneo la Woodvale Groove kaunti ndogo ya Westlands, Nairobi.

Wawili hao walikanusha shtaka la kumteka nyara Koplo Sambach na kuzuia polisi wakiwakamata.

Washtakiwa hao waliomba mahakama iwaachilie kwa dhamana.

Kiongozi wa mashtaka Anderson Gikunda hakupinga washtakiwa hao wakiachiliwa kwa dhamana.

Hakimu mkuu Wendy Kagendo Michemi alielezwa washtakiwa hao walikuwa na lengo la kumtendea unyama afisa huyo wa polisi.

“Naomba mahakama ituachilie kwa dhamana isiyo ya kiwango cha juu,” Kinyua aliirai mahakama.

Kila mmoja aliachiliwa kwa dhamana ya Sh300,000 pesa taslimu.

Kesi itatajwa Aprili 1, 2022.

  • Tags

You can share this post!

Maumau wawasilisha kesi kortini wakitaka Ruto atimuliwe...

Polisi wakana kuhujumu ushahidi katika kesi ya Obado

T L