• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Fahamu nani atakutana na nani kwenye droo kali ya hatua ya 16-bora ya Euro

Fahamu nani atakutana na nani kwenye droo kali ya hatua ya 16-bora ya Euro

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

UINGEREZA watavaana na Ujerumani ugani Wembley mnamo Juni 29 kwenye hatua ya 16-bora ya Euro huku Wales wakichuana na Denmark mnamo Juni 26 jijini Amsterdam, Uholanzi.

Uingereza ya kocha Gareth Southgate ilifuzu baada ya kukamilisha kampeni za Kundi D kileleni huku Ujerumani wakiambulia nafasi ya pili kwenye Kundi F nyuma ya mabingwa wa dunia, Ufaransa.Wales walikamilisha kampeni za Kundi A katika nafasi ya pili nyuma ya Italia walishinda mechi zao zote. Italia watakutana sasa na Austria kwenye muondoano.

DROO YA 16-BORA EURO:

Jumamosi:

Wales vs Denmark – Amsterdam (7:00pm)

Italia vs Austria – Wembley (10:00pm)

Jumapili:

Uholanzi vs Jamhuri ya Czech  (7:00pm)

Ubelgiji vs Ureno – Seville (10:00pm)

Jumatatu:

Croatia vs Uhispaia – Copenhagen (7:00pm)

Ufaransa vs Uswisi – Bucharest (10:00)

Jumanne:

Uingereza vs Ujerumani – Wembley (7:00pm)

Uswidi vs Ukraine – Glasgow (10:00pm)

 

  • Tags

You can share this post!

Ujerumani kuonana na Uingereza huku Ureno wakipepetana na...

Wavuvi washauriwa wawe waangalifu msimu wa mvua