Na MASHIRIKA
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO
UINGEREZA watavaana na Ujerumani ugani Wembley mnamo Juni 29 kwenye hatua ya 16-bora ya Euro huku Wales wakichuana na Denmark mnamo Juni 26 jijini Amsterdam, Uholanzi.
Uingereza ya kocha Gareth Southgate ilifuzu baada ya kukamilisha kampeni za Kundi D kileleni huku Ujerumani wakiambulia nafasi ya pili kwenye Kundi F nyuma ya mabingwa wa dunia, Ufaransa.Wales walikamilisha kampeni za Kundi A katika nafasi ya pili nyuma ya Italia walishinda mechi zao zote. Italia watakutana sasa na Austria kwenye muondoano.
DROO YA 16-BORA EURO:
Jumamosi:
Wales vs Denmark – Amsterdam (7:00pm)
Italia vs Austria – Wembley (10:00pm)
Jumapili:
Uholanzi vs Jamhuri ya Czech (7:00pm)
Ubelgiji vs Ureno – Seville (10:00pm)
Jumatatu:
Croatia vs Uhispaia – Copenhagen (7:00pm)
Ufaransa vs Uswisi – Bucharest (10:00)
Jumanne:
Uingereza vs Ujerumani – Wembley (7:00pm)
Uswidi vs Ukraine – Glasgow (10:00pm)