• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 7:50 AM
Gavana: Toeni fungu la 10

Gavana: Toeni fungu la 10

NA TOM MATOKE

GAVANA wa Nandi, Stephen Sang amewaamuru maafisa wakuu katika serikali yake kupeana asilimia 10 ya mishahara yao kwa makanisa na familia masikini.

Bw Sang alieleza kuwa amewalazimisha maafisa wake kulipa fungu la kumi baada yake kuanzisha makanisa katika kaunti hiyo yanayohitaji msaada kutoka kwa viongozi wa mashinani na wale wa serikali.

“Maafisa wakuu wanaohudumu katika muhula wa mwisho wa serikali yake sharti wawe tofauti kwa kusaidia jamii,” akasema.

Agizo hilo jipya kutoka kwa Gavana Sang lililotolewa wakati wa kuapishwa kwa maafisa hao wapya liliwashangaza.

Hata hivyo haijulikani, jinsi agizo hilo litakavyotekelezwa kwa sababu utoaji fungu la kumi, kwa mujibu wa Bibilia takatifu, ni swala la hiari na wala si la kushurutishwa.

Maafisa hao wakuu wapywa waliapishwa katika afisi za Kaunti ya Nandi mjini Kapsabet Jumatatu.

  • Tags

You can share this post!

Shinikizo kwa Ruto, Raila wazungumze

Azimio yawasilisha kwa mkuu wa polisi Nairobi barua ya...

T L