NA RICHARD MUNGUTI
ALIYEKUWA Gavana wa Samburu, Moses Lenolkulal amepata pigo kubwa baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji kubadili nia na kuamuru kesi inayomkabili ya kujipatia kwa njia ya ufisadi Sh84 milioni kutoka jimbo hilo iendelee.
DPP alikuwa ameamuru kesi hiyo ifutiliwe mbali.