• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
KDF waua magaidi wawili wa al-Shabab

KDF waua magaidi wawili wa al-Shabab

Na KALUME KAZUNGU

WANAJESHI wa Kenya waliwaua magaidi wawili wa kundi la al-Shabaab kwenye operesheni maalum katika msitu wa Boni, Kauti ya Lamu.

Kamishna wa kaunti hiyo, Bw Irungu Macharia, alisema wawili hao waliuawa na maafisa wa usalama kwenye Operesheni ya Linda Nchi katika eneo la Mangulo, Mararani, ndani ya msitu huo.

Alisema washukiwa waliuawa na maafisa hao walipokuwa wakishika doria eneo hilo.

Bw Macharia alisema operesheni zaidi inaendelea kuwafurusha magaidi waliojificha kwenye msitu huo.

“Leo (Jumamosi) asubuhi, wanamgambo wawili wa kundi la al-Shabaab walipigwa risasi na kuuawa na vikosi vya usalama vinavyoendesha Operesheni ya Linda Amani katika msitu wa Boni. Operesheni hiyo bado inaendelea katika msitu huo,” akasema Bw Macharia.

Aliwaomba wananchi kuwa macho na kuripoti mtu yeyote wanayetilia shaka mienendo yake kwa vikosi vya usalama.

Duru za kiusalama ziliiambia Taifa Jumapili kwamba kisa hicho kilifanyika mwendo wa kumi kasorobo alfajiri.

  • Tags

You can share this post!

Magavana wadai Jubilee ina nia ya kuua ugatuzi

Viongozi wataka kaunti 8 za Mashariki kuungana