Na WANGU KANURI
KAMPUNI ya Kenya Power imewahakikishia Wakenya kuwa wahandisi wanashughulika kuhakikisha kuwa stima zimerejea haraka iwezekanavyo.
Hii ni baada ya sehemu kadhaa nchini kukosa stima Jumanne asubuhi.
“Ukosefu huo umeshuhudiwa baada ya minara miwili kuangukia vipitisho vya stima vya Kiambere na Embakasi saa tano kasorobo asubuhi,” taarifa ya Kenya Power imesema.
Hata hivyo, licha hakikisho hilo lililosambaratisha shughuli za kawaida za utendakazi, ni sehemu nyingi nchini zilizoathirika.
Kampuni hiyo imekuwa ikimulikwa mara kadhaa kwa utepetevu wake wa kusitiri vikingi na nyaya za stima.
Baadhi ya waathirika hutumia majukwaa ya mitandao ya kijamii kuelezea kero zao.