NA GEORGE MUNENE
KIZAAZAA kilizuka katika Kaunti ya Embu, mlanguzi wa dawa za kulevya kutoka kijiji cha Gakwegori alipowasihi polisi wasimkamate kwa kupanda bangi anayotumia kwa matumizi yake ya kibinafsi.
“Ninatumia bangi kunisisimua tu. Msinipeleke kwenye kituo cha polisi,” mshukiwa alisihi.
Naibu Kamishna wa Kaunti ya Embu Magharibi, Bw Charles Opiyo alionya kuwa watakaopatikana wakifanya biashara haramu watachukuliwa hatua.
“Ni kosa la jinai kukuza bangi au kufanya biashara hiyo. Napongeza wakazi kufichua hili,” akasema Bw Opiyo.