Na KNA
GAVANA wa Kwale, Bw Salim Mvurya (pichani), amewashauri wazazi kuwa waangalifu kwa watoto wao wasije wakasombwa na mafuriko.
Alisema hayo akiomboleza na familia za watoto ambao walifariki Jumatatu katika mto Mwache.
Miili ya watoto wawili kati ya watatu waliozama ilipatikana, na kufikia Jumatano, juhudi za kumtafuta mtoto wa tatu zilikuwa bado zinaendelea.