NA WINNIE ATIENO
WAZIRI wa usalama, Dkt Fred Matiang’i, ameonya kuna wanasiasa katika kaunti mbili za Pwani wanaopanga kutumia magenge ya wahalifu kutatiza uchaguzi Agosti 9, 2022.
Akizungumza Mombasa mnamo Jumatano baada ya kukutana na maafisa wa usalama pamoja na Inspekta Jenerali Hilary Mutyambai, aliagiza polisi wasihurumie mwanasiasa atakayepatikana akifadhili magenge ya uhalifu.
Alisema idara ya polisi itatuma maafisa zaidi na rasilimali nyingine za usalama Pwani hivi karibuni kabla siku ya uchaguzi ifike.