• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 10:50 AM
Matiang’i aonya viongozi dhidi ya kufadhili magenge Pwani

Matiang’i aonya viongozi dhidi ya kufadhili magenge Pwani

NA WINNIE ATIENO

WAZIRI wa usalama, Dkt Fred Matiang’i, ameonya kuna wanasiasa katika kaunti mbili za Pwani wanaopanga kutumia magenge ya wahalifu kutatiza uchaguzi Agosti 9, 2022.

Akizungumza Mombasa mnamo Jumatano baada ya kukutana na maafisa wa usalama pamoja na Inspekta Jenerali Hilary Mutyambai, aliagiza polisi wasihurumie mwanasiasa atakayepatikana akifadhili magenge ya uhalifu.

Alisema idara ya polisi itatuma maafisa zaidi na rasilimali nyingine za usalama Pwani hivi karibuni kabla siku ya uchaguzi ifike.

  • Tags

You can share this post!

Hisia mseto Sri Lanka ikipata rais mpya

Ruto anamhemesha Raila hapa Pwani, Kingi asema

T L