• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:35 AM
Mbakaji aliyenajisi kanisani asukumwa jela miaka 45

Mbakaji aliyenajisi kanisani asukumwa jela miaka 45

NA RICHARD MUNGUTI

MWANAMUME aliyembaka msichana mwenye umri wa miaka miwili katika Kanisa moja eneo la Zimmerman, Nairobi amehukumiwa kifungo cha miaka 45 bila faini gerezani.

Erastus Kariuki, 39 ataondoka Gereza kuu la Kamiti alikopelekwa kutumikia kifungo akiwa na umri wa miaka 84.

Akipitisha hukumu, hakimu mwandamizi Mahakama ya Milimani, Bi Wandia Nyamu alisema mshtakiwa alimtendea unyama msichana huyo mdogo Kanisani.

Bi Nyamu alisema uhalifu aliotenda Kariuki umemfanya atengwe na jamii ambapo uhuru wa wanawake na wasichana unashabikiwa.

“Hii mahakama haitakukubalia utangamane tena na wananchi wapenda amani. Itabidi utengwe kwa miaka 45,” alisema Bi Nyamu akipitisha hukumu.

Hakimu alisema mshtakiwa alienda katika kanisa hilo lililoko Zimmerman na kutoa mchango wa Sh100 alioutumia kama kibali cha kumvizia mlalamishi.

Hakimu alifahamishwa mshtakiwa alimkabidhi Pasta mchango wake kisha akaondoka kanisani.

Aliwasongea wasichana waliokuwa wanacheza nje ya Kanisa baada ya Ibada.

Mshtakiwa alimwita msichana huyo na alipomsongea akamshika na kumfunika mdomo huku akitoroka naye.

Mayowe ya msichana huyo yalimfikia mama yake. Mshtakiwa alikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi cha Kasarani alipozuiliwa na msichana kupelekwa hospitali kutibiwa.

  • Tags

You can share this post!

KINYUA BIN KING’ORI: Bei ya unga isalie Sh100 hata...

GWIJI WA WIKI: Mathias Momanyi

T L