• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:07 PM
Mke anataka kuniacha sababu mimi ni mkulima

Mke anataka kuniacha sababu mimi ni mkulima

SHANGAZI;

Niliachishwa kazi mapema mwaka huu. Kwa bahati nzuri, nilikuwa nimeanza biashara ya kilimo na imenawiri. Lakini mke wangu anatishia kuniacha akisema hakutarajia kuolewa na mkulima. Nifanye nini?

Msimamo wa mke wako ni duni. Kazi ni kazi bora pesa. Asilimia kubwa ya matajiri maarufu duniani ni wakulima. Kama shabaha yake ni mume wa kufunga tai, achana naye akatafute. Utapata mwingine anayeelewa maana ya kazi.

Mama mkwe anichukia sana licha ya kumpenda

Nimeolewa kwa miaka miwili. Mama yangu mzazi aliaga dunia kwa hivyo namchukulia mama mkwe kama mama yangu. Lakini ananichukia sana. Nifanye nini?

Ni hali ya kuvunja moyo kwamba mama mkwe analipa wema na heshima yako kwake kwa chuki. Lakini usiache kumpenda, kumheshimu na kumtendea wema. Huenda siku moja akabadili nia yake kwako.

Aliniacha akaoa mwingine, bado nampenda, ushauri?

Nimezaa mtoto na mpenzi wangu. Nilikuwa na matumaini makubwa kuwa atanioa lakini ameoa mwanamke mwingine. Nampenda sana na yuko tayari tuendelee kuwa wapenzi. Waonaje?

Sijui ni kwa nini unapoteza wakati wako kwa mwanamume ambaye hana mpango wowote kwa maisha yako. Hatua yake ya kuoa mwanamke mwingine imethibitisha kuwa hakupendi. Achana naye utafute wako.

Bosi anahemea penzi langu lakini mimi tayari ni mke wa mtu, naogopa

Bosi wangu kazini ananitaka kimapenzi. Siwezi kukubali ombi lake kwa sababu ana mke. Isitoshe, uhusiano wetu utaniletea aibu miongoni mwa wafanyakazi wenzangu. Nifanyeje?

Naunga mkono kikamilifu msimamo wako. Kimaadili, uhusiano wako na bosi wako unafaa kuwa wa kikazi tu. Mbali na aibu kazini, habari za uhusiano wenu zitamfikia mke wake na utajipata mashakani. Usikubali.

  • Tags

You can share this post!

Wabunge wakataa wasichana matineja wasipewe tembe za kuzuia...

‘Makosa’ ya utawala wa Kenya Kwanza...

T L