• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Naona aibu kumwambia mwanaume jirani yangu kuwa nampenda

Naona aibu kumwambia mwanaume jirani yangu kuwa nampenda

SHANGAZI;

Naumia sana moyoni kwa mapenzi ya mwanamume jirani yangu mtaani. Najua si kawaida ya mwanamke kumtongoza mwanamume lakini mimi sijali. Nimeshindwa kumwambia ingawa tumekuwa tukikutana kila mara. Nifanyeje?

Unaumia moyoni kuhusu mtu ambaye hana habari kuhusu unavyohisi. Ni kweli, si kawaida kwa mwanamke kumtongoza mwanamume. Lakini pia si hatia kufanya hivyo. Jinsi pekee ya kujua kama yeye pia anakupenda ni kumwambia. Usingoje kisha baadaye ujute akinyankuliwa na mwingine.

Dume lanitongoza ilhali huchovya buyu la mdada rafiki yangu

Kuna mwanamume amekuwa akiniandama kwa mwaka mzima sasa akitaka tuwe wapenzi. Najua kuwa ni mpenzi wa rafiki yangu lakini sitaki kumwambia kwani itakuwa aibu kwake. Nishauri.

Mwanamume huyo haoni aibu kukutongoza ilhali ni mpenzi wa rafiki yako. Mbona wewe unaona aibu kumwambia? Kama hutaki aendelee kukusumbua, itabidi umwambie ukweli.

Ataka niwe mpango wa kando, si mke wa 2

Nina miaka 30 na nina mtoto. Baba ya mtoto wangu aliniacha baada ya kunipa mimba. Natamani sana kuolewa lakini mwanamume anayenitaka ana familia. Anataka niwe mpango wa kando na ameniahidi kunitunza kama mke wake. Nipe ushauri.

Nia yako hasa ni kuolewa. Mwanamume huyo asikudanganye eti atakutunza kama mke wake. Wajibu wa kwanza wa mwanamume aliyeoa ni kwa familia yake.Wewe bado ni mwanamke mchanga. Kuwa na subira, utapata mume wako mwenyewe.

Alinionya eti sitapata mpenzi nilipomkataa

Kuna mwanamume aliyenitaka kimapenzi lakini nikamkataa kwa sababu sikuwa na hisia kwake. Alikasirika sana na akanionya kuwa sitawahi kupata mpenzi. Huu ni mwaka wa pili na bado sijapata. Nina wasiwasi.

Hakuna binadamu aliye na uwezo katika maisha yako. Ondoa mawazo hayo akilini mwako na uendelee kutafuta. Wakati ukifika utampa mpenzi anayestahili moyo wako.

  • Tags

You can share this post!

Mikakati ya serikali kuzima visa vya utekaji nyara nchini

Watalii kulipa kibunda cha pesa kupata idhini ya kupiga...

T L