• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:55 AM
Nyumba za kisasa kujengwa Ruiru na Thika

Nyumba za kisasa kujengwa Ruiru na Thika

Na LAWRENCE ONGARO

WAKAZI wa Ruiru watanufaika kwa ujenzi wa nyumba 500 eneo la Majengo karibu na soko kuu la eneo hilo.

Gavana wa Kiambu, Dkt James Nyoro, alieleza kuwa mji wa Ruiru unastahili kujengwa nyumba za kisasa kutokana na ongezeko la watu.

Alieleza kuwa nyumba za hapo awali zilijengwa zaidi ya miaka 50 iliyopita na kwa hivyo tayari zimepoteza umuhimu wake.

Wakati huo pia alieleza kuwa nyumba zote zilizojengwa na manispaa ya hapo awali ya Thika, zitafanyiwa ukarabati ili ziwe katika hali ya kisasa.

Nyumba hizo in zile za Depot, na Jamafosa zilizoko mjini Thika.

“Tunaelewa nyumba hizo zilijengwa zamani na kwa hivyo zimepoteza uzuri wake. Kwa hivyo ni vyema kujenga nyingine mpya za kisasa,” alisema Dkt Nyoro.

Alitoa wito kwa wawekezaji wajitokeze mjini Thika ili waweze kupata nafasi ya kujenga nyumba katika ardhi ya ekari 23.

Aliyasema hayo mjini Thika mnamo Alhamisi alipohudhuria hafla iliyojumuisha zaidi ya vyuo vya masomo 10 vilivyofika katika uwanja wa Mama Ngina ili kuonyesha baadhi ya kozi wanazosoma kwa mwongozo unaotangazwa kama (Smart Education Expo), iliyohudhuriwa na vyuo tofauti na wawakilishi wao.

Zaidi ya vyuo vya mafunzo 10 vilihudhuria ikiwemo Mount Kenya, Zetech, na Cascade miongoni mwa vingine.

Alisema wanafunzi wengi waliokamilisha elimu ya sekondari walitarajiwa kuhudhuria hafla hiyo ili wapate mwongozo wa kujichagulia masomo watakayochagua watakapojiunga na vyuo hivyo.

Alithibitisha kuwa kwa mwaka mmoja na nusu uliosalia serikali ya Kaunti ya Kiambu itafanya juhudi kuona ya kwamba mji wa Thika iumepiga hatua ili kuona ya kwamba Ajenda Nne muhimu za serikali ya kitaifa ambapo ujenzi wa nyumba mpya unahusika, zinatimizwa kabla ya mwaka mmoja na nusu ujao.

You can share this post!

Wilfried Zaha awataka Palace wamwachilie atafute hifadhi...

Faida ndani ya chai ya hibiscus