• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 9:50 AM
Papa Francis amteua askofu mpya Bungoma

Papa Francis amteua askofu mpya Bungoma

Na BRIAN OJAMAA

PAPA Francis amemteua Kasisi Monsignor Mark Kadima, kuwa askofu mpya wa Dayosisi ya Kanisa Katoliki ya Bungoma.

Kaasisi huyo aliteuliwa kuhudumu katika nafasi hiyo mpya kulingana na tangazo lililochapishwa na jarida la L’Osservatore Romano, jijini Roma, Jumanne.

Tangazo hilo limeibua msisimko wa aina yake katika dayosisi hiyo huku washiriki wengi wakielezea furaha yao.

Ni uteuzi ambao pia ulitolewa na mwakilishi wa Papa nchini Kenya na Sudan Kusini, Askofu Bert Van Megen, kwenye taarifa aliyotuma kwa Muungano wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki Kenya (KCCB).

“Nina furaha kuwafahamisha kuwa Papa Francis amemteua Kasisi Monsignor Mark Kadima kuwa Askofu wa Bungoma,” akasema.

Dayosisi hiyo imekuwa ikiongozwa na Askofu Joseph Obanyi wa Dayosisi ya Kakamega.

You can share this post!

Korti yaondoa agizo la Kinoti kutupwa jela

Pigo kwa Ruto wakati Obado akihama ‘Tangatanga’

T L