Na IAN BYRON
NAIBU Rais William Ruto amepata pigo eneo la Nyanza, baada ya Gavana Okoth Obado wa Migori kuhama kambi ya ‘Tangatanga.’
Kwenye hatua ambayo imewashangaza wengi, Bw Obado alisema hatashirikiana tena na Dkt Ruto, licha ya kuandamana naye kwenye mikutano kadhaa aliyofanya katika eneo hilo mnamo Septemba.