• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Raila amwomboleza mwanahabari shupavu Philip Ochieng’

Raila amwomboleza mwanahabari shupavu Philip Ochieng’

Na CHARLES WASONGA

KIONGOZI wa ODM Raila Odinga ameomboleza kifo cha mwanahabari mkongwe Philip Ochieng’ akimtaja kama mtaalamu aliyechochea mabadiliko katika jamii kupitia kazi zake.

Kupitia ujumbe katika akaunti zake za mtandao wa kijamii, Bw Odinga alisema Kenya imempoteza mwanahabari wa kupigiwa mfano na mwenye ufasaha katika lugha ya Kiingereza.

“Kupitia weledi wake katika uandishi, Philip aliongelesha watu wetu mamlaka makuu na kuwafanya wanajamii kuchua hatua mbali mbali zenye faida kwa. Alikuwa mwalimu na mshauri wa jamii kupitia kazi zake,” Waziri huyu mkuu wa zamani akasema.

“Philip aliandika mawazo yake na kuwapa sauri wale wasio na usemi. Natuma rambirambi zangu kwa familia na marafiki na jamii ya wanahabari kwa ujumla. Mungu aiweke roho yake pema penye amani,” Bw Odinga akaongeza.

Naibu Rais pia aliwasilisha rambirambi zake akimtaja marehemu Ochieng’ kama mwanahabari ambaye alikuwa na uelewa mpana wa masuala katika nyanja zote za maisha.

“Alikuwa mweledi katika sarufi ya kiingereza na alikuwa nafasi yake magazeti ambapo alitufunza mambo mapya kila mara. Ochieng’ ni mwanahabari msomi ambaye alielimisha wanajamii kupitia makala yake. Mungu aiweke roho yake pema pema wema,” akasema Dkt Ruto.

Familia ya marehemu Ochieng ilithibitisha kuwa mwanahabari huyo mweledi alifariki nyumbani kwake Awendo, kaunti ya Migori baada ya kuugua ugonjwa wa “pneumonia”.

Marehemu alikuwa alikuwa akiandika makala katika gazeti la Sunday Nation ambapo alitumia lugha ya kipekee ya Kiingereza. Makala yake ilijulikana kama “The Fifth Columnist”.

Miaka mingi hapa nyuma marehemu Ochieng’ alihudumu kama mhariri wa magazeti ya Daily Nation na Sunday Nation.

You can share this post!

LEONARD ONYANGO: Magavana waliofuja fedha za corona...

Tunapoweka mikakati ya kuboresha kilimo tusisahau kuinua...