MARY WANGARI na PSCU
RAIS Uhuru Kenyatta jana aliifariji familia ya Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee, Waziri Raphael Tuju, kufuatia kifo cha mamake, Mary Odiyo Tuju.
Bi Odiyo aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 87, usiku wa kuamkia jana, alipokuwa akipokea matibabu katika Nairobi Hospital.
Katika rambirambi zake za kuifariji familia na jamaa, rais alimtaja Mamake Waziri Tuju kama kiongozi wa jamii aliyekuwa na bidii na mama mkarimu aliyethamini elimu kama msingi wa maisha.
“Mama Mary alikuwa kiongozi aliyejulikana na kuheshimika sana ambaye aliamini katika maadili na manufaa ya elimu,” alisema Rais.