• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Rooney afanyiwa ‘ile kitu’ sasa yeye ni gumegume bila uwezo wowote!

Rooney afanyiwa ‘ile kitu’ sasa yeye ni gumegume bila uwezo wowote!

Na CHRIS ADUNGO

TOFAUTI na wanawake walio na mbinu tele za kuzuia mimba, wanaume hutegemea njia mbili pekee — mipira ya kondomu au kukatwa mrija wa kupitisha mbegu za uzazi, kwa Kimombo vasectomy.

Mke wa mwanasoka mstaafu Wayne Rooney, Coleen, amefichua kwamba mumewe sasa hawezi tena kumtunga mwanamke mimba kwa kuwa amefanyiwa vasectomy.

Katika mahojiano na gazeti la The Sun wiki hii, Coleen alikiri kumshawishi nyota huyo wa zamani wa Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza, kuendea mbinu hiyo ya upangaji uzazi kwa wanaume.

“Alifanyiwa upasuaji huo baada ya mtoto wetu wa nne kuzaliwa. Nilizungumza na Rooney na akaona umuhimu wa vasectomy ili tusipate mtoto mwingine,” alitanguliza Coleen, 37.

Cass, aliye na umri wa miaka mitano, ndiye kitinda mimba wa Rooney na Coleen.

Wanandoa hao wamejaliwa watoto wanne — Kai, 13, Klay, 10, Kit mwenye umri wa miaka saba na Cass.

“Kila mara nilipojifungua, wanahabari walifanya mazoea kuniuliza iwapo ningeendelea kupata watoto. Swali gumu zaidi walilotaka nijibu ni iwapo nilitamani kupata mtoto wa kike,” akasema Coleen.

“Tamanio langu lilikuwa kupata watoto wachache, kama watatu hivi. Lakini nilishawishika kutafuta binti baada ya kumzaa Kit. Nilifadhaika sana ilipotokea kuwa mtoto wetu wa nne pia ni mvulana,” akaeleza.

“Nilimzungumzia Rooney kwa ukali sana na akakubali pendekezo langu la kupanga uzazi. Sikutaka mimba nyingine na akakubali kuonja makali ya kisu,” aliongeza.

Rooney, 37, alipendana na Coleen tangu wakiwa na umri wa miaka 16 kisha wakafunga ndoa 2008.

Sogora huyo wa zamani wa Everton na DC United sasa ni kocha wa Birmingham City.

Amewahi kukwaruzana na mkewe mara kwa mara kuhusu michepuko na unywaji pombe kupindukia.

  • Tags

You can share this post!

Aliua mwanawe ili apate nafasi ya kuyoyomea Uarabuni lakini...

Waziri Mkuu wa Italia amtema mchumba wake kwa kauli zake za...

T L