• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 5:17 PM
TSC yachunguza mwalimu kwa dai la uporaji wa pesa

TSC yachunguza mwalimu kwa dai la uporaji wa pesa

Na KNA

TUME ya Kuajiri Walimu (TSC) imeanza kumchunguza mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi ya Mwania katika kaunti ndogo ya Kathozweni, Kaunti ya Makueni, kufuatia madai ya matumizi mabaya ya fedha.

Mkurugenzi wa TSC Kaunti ya Makueni, Bw Alex Cheruiyot, alisema maafisa wa Idara ya Uhasibu wametumwa kuchunguza jinsi pesa za shule hiyo zimetumika, baada ya wazazi kuandamana Jumatatu.

Bw Cheruiyot aliongeza kuwa tayari mwalimu huyo mkuu amepewa barua kuhusiana na malalamishi hayo.

“Tuliomba mhasibu wa shule kufanya uchunguzi hata kabla ya wazazi kuanza kulalamika. Tuko na ripoti na tunafuata mchakato unaofaa kubaini ukweli wa madai hayo,” alieleza Jumanne ofisini mwake mjini Wote.

  • Tags

You can share this post!

Taita Taveta yapeleka zogo la ardhi mahakamani

Kosgey ahimizwa awanie kiti cha useneta Nandi