NA KENYA NEWS AGENCY
KAUNTI ya Siaya imepiga hatua katika vita dhidi ya Ukimwi baada ya maambukizi mapya kupungua kwa asilimia 84 kwa matineja wa kati ya umri wa miaka 10-19.
Kupungua kwa maambukizi hayo ni kutoka mnamo 2015 hadi 2021.
Kwa mujibu wa Lucy Ghati, Mkurugenzi wa Baraza la Kudhibiti Magonjwa (NSDCC) idadi ya maambukizi mapya sasa ni 371 kutoka watu 2,355.
Alikuwa akizungumza mjini Siaya wakati wa hamasisho dhidi ya Ukimwi linalolenga kupunguzwa kwa maambukizi mapya.