• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Vihiga Queens na Thika Queens walishinda zoni zao za Ligi Kuu ya Wanawake

Vihiga Queens na Thika Queens walishinda zoni zao za Ligi Kuu ya Wanawake

Na GEOFFREY ANENE

MABINGWA watetezi Vihiga Queens na washindi wa zamani Thika Queens wamekamilisha msimu wa kawaida wa Ligi Kuu ya Wanawake bila kupoteza katika Zoni B na A mnamo Jumamosi, mtawalia.

Vihiga wamechabanga nambari nne Trans Nzoia Falcons 3-2 katika uwanja wa Kodiaga Prison mjini Kisumu nao Thika wamelipua Mathare United wanaokamata mkia 5-0 ugani Camp Toyoyo mjini Nairobi.

Vipusa wa kocha Alex Alumira, ambao walishinda Ligi Kuu mwaka 2017, 2018 na 2019, wametawala Zoni B kwa alama 40. Walizoa ushindi mara 13 na kutoka sare mchuano mmoja. Nakuru West Queens walikung’uta SEP Oyugis 2-0 kumaliza msimu katika nafasi ya pili kwa alama 27 nao Wadadia wakaridhika na nafasi ya tatu kwa alama 26 baada ya kukabwa 1-1 dhidi ya Kisumu All Starlets.

Thika walishinda michuano yao yote 14. Walifuatiwa na Gaspo Women waliozoa alama 29 baada ya kulazimishiwa sare ya 3-3 dhidi ya nambari mbili kutoka mwisho Makolanders. Ulinzi Starlets iliridhika na nafasi ya tatu kwa alama 28 baada ya kutoka sare tasa dhidi ya Zetech Sparks. Timu hizo tatu za kwanza kutoka makundi hayo mawili zimefuzu kushiriki mashindano ya kuamua mshindi.

Matokeo (Juni 12):

Vihiga Queens 3-2 Trans Nzoia Falcons

Zetech Sparks 0-0 Ulinzi Starlets

Nakuru Queens 2-0* SEP Ladies

Mathare United Women 0-5 Thika Queens

Kibera Soccer Ladies 1-2 Kayole Starlet

Wadadia 1-1 Kisumu All Starlets

Gaspo 3-3 Makolanders

  • Tags

You can share this post!

Sijapata hakikisho mastaa wa Kenya Simbas watashiriki mechi...

Chipu yapasua Mwamba raga ya kujiandalia Kombe la Afrika