• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Wanawake 3 wafungwa jela miezi sita kwa kuiba simu ya mwanamume

Wanawake 3 wafungwa jela miezi sita kwa kuiba simu ya mwanamume

WANAWAKE watatu waliomwibia mkulima simu alipolewa katika kilabu kimoja jijini Nairobi wamefungwa miezi sita kila mmoja.

Rachel Wanjiru Kinyanjui, Nelius Muthoni Njahi na Georgina Wawira Muthoni walifungwa na hakimu mkuu mahakama ya Nairobi Wendy Kagendo.

Wanjiru, Muthoni na Wawira walikiri walimwibia John Kinyua Njeru simu muundo wa Tecno Spark iliyo na thamani ya Sh16,000.

Licha ya kumlipa Njeru simu yake “hakimu alisema washtakiwa hao walifanya uhalifu kwa kuiba simu.”

Washtakiwa hao walimweleza hakimu walificha simu hiyo ndani ya choo lakini haikuweza kupatikana.

“Mheshimwa tumechanga pesa na tuko tayari kumlipa mshtakiwa,” Wawira alimweleza hakimu.

Pia Wawira alisema Wanjiru ndiye alimwibia Njeru simu hiyo kisha akampa Nelius ailinde.

Wawira pia aliichukua lakini akamrudishia Nelius.

Wote watatu walikiri kushirikiana kuiba simu hiyo.

Mahakama ilifahamishwa polisi kwa msaada wa kampuni ya Safaricom walipata mawimbi – signals – ya simu hiyo katika eneo la Kariobangi, Nairobi.

Watatu hao walikiri kuiba simu hiyo mnamo Machi 3, 2022 katika kilabu cha Eureka kilichoko barabara ya Tom Mboya.

  • Tags

You can share this post!

11 kupambana mmoja wao awe mgombea mwenza wa Raila

Brighton yadhalilisha Man-United katika pambano la EPL...

T L