• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 5:04 PM
Wanawake watatu waokolewa msituni Shakahola

Wanawake watatu waokolewa msituni Shakahola

NA ALEX KALAMA

LEO Jumanne, takriban wanawake watatu wameokolewa kwenye msitu wa Shakahola ulioko katika Kaunti ya Kilifi.

Mwanamke mmoja amepatikana na kuokolewa katika msitu wa Shakahola akiwa anatembea kwa barabara.

Alijaribu kutoroka ili kuvuka ng’ambo ya pili ya barabara hiyo kukwepa kuokolewa na maafisa wa polisi wanaoendesha operesheni kwenye shamba linalodaiwa kumilikiwa na mhubiri Paul Mackenzie.

Mwanamke huyo alifunika uso wake kwa nguo hivyo wanahabari wanaopiga picha hawakunasa sura yake vizuri.

Hao wanawake wengine wawili nao wameokolewa baada ya kupatikana wakiwa katika hali mbaya ndani ya nyumba kwenye msitu huo wakiendeleza mfungo wao.

Wanawake wawili wameokolewa baada ya kupatikana wakiwa katika hali mbaya ndani ya nyumba kwenye msitu wa Shakahola wakiendeleza mfungo wao. PICHA | WACHIRA MWANGI

Maafisa wa polisi wakishirikiana na mashirika ya kutetea haki za binadamu pamoja na Shirika la Msalaba Mwekundu na kukimbizwa katika hospitali kuu ya Malindi ili kupata matibabu ya dharura.

  • Tags

You can share this post!

Fahamu kwa nini stima ingali ghali

Hakuna muda wa kulala Arsenal wakielekea uwanjani Etihad

T L