• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 9:50 AM
Watu 13 wajeruhiwa katika shambulizi

Watu 13 wajeruhiwa katika shambulizi

NA MASHIRIKA

AUSTIN, AMERIKA

WATU wasiopungua 13 walijeruhiwa, wawili miongoni mwao wakiachwa hali mahututi, katika kisa cha ufyatuaji risasi kilichotokea jana kwenye jimbo la Austin, Texas.

Milio ya risasi ilizuka kabla tu ya saa saba na dakika ishirini na tano usiku kwenye mtaa wa Sixth Street, eneo lililojaa vilabu na hoteli.Barabara hiyo ilifungwa ili kuzuia magari kupita shambulizi hilo lilipokuwa likifanyika, kwa mujibu wa Kaimu Afisa Mkuu wa Polisi, Austin, Joseph Chacon.

“Maafisa wetu walichukua hatua haraka,”“Waliweza kuanza mara moja shughuli za kuokoa maisha ya wahasiriwa wengi, ikiwemo matumizi ya vifaa muhimu na vifuniko vya vifua,” alisema.

Mshambulizi hakukamatwa mara moja huku kiini cha shambulizi hilo kikiwa hakijulikani.

  • Tags

You can share this post!

Mwanaharakatiaachiliwa kabla ya kukamilisha kifungo

Mabalozi wafukuzwa kwa kuuza pombe