• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Mwanaharakatiaachiliwa kabla ya kukamilisha kifungo

Mwanaharakatiaachiliwa kabla ya kukamilisha kifungo

Na Mashirika

MWANAHARAKATI mashuhuri wa kupigania demokrasia Hong Kong, Agnes Chow, aliachiliwa gerezani jana baada ya kutumikia karibu miezi saba ya kifungo chake cha miezi 10.

Alilakiwa na wafuasi wake na vyombo vya habari lakini akasafirishwa kwa gari bila kutoa kauli yoyote.Serikali nchini humo haikusema ni kwa nini aliachiliwa huru kabla ya kifungo chake kukamilika.

Chow na wanaharakati wenzake Joshua Wong na Ivan Lam, walifungwa jela mwaka uliopita kwa sababu ya mchango wao katika maandamano ya 2019.Uchina baadaye ilitangaza sheria kuhusu usalama wa kitaifa ili kunyamazisha malalamishi Hong Kong.Chow, 24, aliondoka kwenye malango ya gereza jana saa nane adhuhuri.

Wafuasi wake walisikika wakiimba ‘Ongeza Mafuta!’ – msemo uliogeuka kaulimbiu wakati wa maandamano hayo ya umma.Chow pamoja na Wong na Lam, ambao vilevile wapo katika miaka yao ya 20 waligeuka sura ya maandamano ya Hong Kong.

 

  • Tags

You can share this post!

Ngarambe ya Copa America yang’oa nanga usiku wa leo

Watu 13 wajeruhiwa katika shambulizi