NA CHARLES WASONGA
WAVULANA wengi walikosa kufanya Mtihani wa Kitaifa wa Kidato cha Nne (KCSE) ikilinganishwa na wasichana, kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa Ijumaa na Waziri wa Elimu, Ezekiel Machogu.
Kulingana takwimu zilizoletwa na Baraza la Kitaifa la Mitihani Nchini (KNEC), jumla ya wavulana 445,103 walisajiliwa kwa ajili ya kuufanya mtihani huo, lakini ni 444,644 waliufanya mwishoni mwa mwaka 2022.
Hii ina maana kuwa, jumla ya watahiniwa 1,459 wa kike walikosa kufanya KCSE licha ya kusajiliwa, na serikali kulipia gharama ya uchapishaji wa karatasi ambazo wangefanya.
Kwa upande mwingine, wasichana 1,247 walikosa kufanya mtihani huo licha ya kusajiliwa. Hii ni kwa sababu jumla ya watahiniwa 439,019 wa kike walisajiliwa lakini ni 437,772 walifaulu kufanya mtihani huo wa KCSE.
Uchunguzi umeonyesha kuwa, baadhi ya watahiniwa hukosa kufanya mitihani ya kitaifa licha ya kusajiliwa kutokana na sababu kadha ikiwa ni pamoja na vifo.
Wakati huo huo, kaunti 14 zilikuwa na watahiniwa wengi wavulana kuliko wale wa kike katika KCSE 2022 ikilinganishwa na kaunti 17 mwaka wa 2021.
Subscribe our newsletter to stay updated