• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Yaya aliyeonjesha mvulana mdogo asali kukaa jela miaka 8

Yaya aliyeonjesha mvulana mdogo asali kukaa jela miaka 8

NA RICHARD MUNGUTI

YAYA mwenye umri wa miaka 34 aliyepatikana na hatia ya kumwingiza mvulana wa mwajiri wake mwenye umri wa miaka 13 katika maisha ya kuchovya asali Alhamisi alisukumwa jela miaka minane.

Mshtakiwa aliyetambuliwa kwa herufi VNW alifungwa na hakimu mwandamizi mahakama ya Milimani Bi Esther Kimilu.

Akipitisha hukumu, Bi Kimilu, alisema mshtakiwa alifanya vibaya kwa vile “mvulana huyo yuko anataka kila siku.”

Mbali na tendo hilo la kujamiiana mshtakiwa pia alikuwa anatazama filamu za ngono na mvulana huyo.

Hakimu alisema akili ya mvulana huyo sasa imekwama kwa tendo la ngono ambalo anataka kufanya kila siku.

Bi Kimilu alisema mvulana huyo anahitaji tiba maalum na ushauri kutoka kwa wataalam ndipo mawazo yake yabadilishwe.

“Upande wa mashtaka umethibitisha kesi dhidi ya mshtakiwa ya kumdhalilisha kingono mvulana wa umri mdogo na uchafuzi wa mawazo ya mlalamishi kwa kutazama filamu za ngono,” Bi Kimilu alisema.

Akijitetea, mshtakiwa alisema aliozwa akiwa na umri wa miaka 14 na walitengana na mumewe.

Hakuweza kuendelea na masomo.

“Mimi ni mama wa watoto wanne na sasa ninasumbuka kuwakimu kimaisha,” alisema mshtakiwa akijitetea.

Aliomba msamaha akisema ameghairi matendo yake na kuomba mahakama imhurumie ili arudie watoto wake.

“Nimetilia maanani malilio ya mshtakiwa. Hii mahakama inazingatia mshtakiwa alimdhulumu kimapenzi mvulana huyo wa umri mdogo,” alisema hakimu.

Mshtakiwa alidaiwa alitekeleza uhalifu huo kwa miaka miwili 2020 na 2021 alipopatikana.

Hakimu alifahamishwa wazazi wa mvulana huyo walitambua mjakazi wao alikuwa anashiriki ngono na mwana wao baada ya binti yao kuripoti simu yake ya smartphone ilikuwa imepotea.

Mvulana huyo alichapwa ndipo akakiri ndiye aliiba simu ya dada yake kutazama picha za ngono jinsi walivyokuwa wakitazama na mshtakiwa.

  • Tags

You can share this post!

Kijana ashtakiwa kwa kumtusi baba na kuiba simu ya mama yake

Jinsi kondomu zilizotupwa kiholela zinavyojenga maudhui...

T L