• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 5:50 AM
Kijana ashtakiwa kwa kumtusi baba na kuiba simu ya mama yake

Kijana ashtakiwa kwa kumtusi baba na kuiba simu ya mama yake

NA RICHARD MUNGUTI

KIJANA wa kiume ameshtakiwa kwa kumtukana baba yake na kuiba simu ya mama yake.

Michael Njenga alikanusha mashtaka hayo mbele ya hakimu mwandamizi Derrick Kutto.

Inadaiwa alimtukana baba yake mzazi matusi meusi na yenye soni ambayo hatuwezi kuyachapisa.

Hakimu alielezwa mshtakiwa alimkejeli baba yake kwa kumweleza hakuweka mipango kabambe kuhusu maisha yake ya usoni alipokuwa mwanarika.

Njenga alikabiliwa na shtaka la kuzua fujo na kuhatarisha amani katika eneo la Magorofani mtaani Langata, Nairobi.

Hakimu alifahamishwa mshtakiwa amekuwa akirudia makosa hayo kila siku.

Alikana kuiba simu ya mama yake Nancy Wamboi iliyo na thamani ya Sh1,500 mnamo Machi 27, 2022.

Mshtakiwa aliachiliwa kwa dhamana ya Sh50,000 pesa taslimu.

Kesi itaanza kusikilizwa Juni 22, 2022.

  • Tags

You can share this post!

Mirema: Dennis Gachoki aachiliwa huru baada ya kukosekana...

Yaya aliyeonjesha mvulana mdogo asali kukaa jela miaka 8

T L