Na ANTHONY KITIMO
WANASIASA wa Pwani wamekashifiwa kwa kutohudhuria kongamano la Jumuiya ya Pwani lililofanyika jana katika Kaunti ya Kwale.
Gavana wa Tana River, Bw Dhadho Godhana (pichani) pekee ndiye kiongozi wa kisiasa aliyekuwepo. Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga aliyetarajiwa kuhudhuria, alihutubia kikao kupitia kwa mtandao akiwa Nairobi.