• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Raia wa Pakistan asababisha kioja kortini

Raia wa Pakistan asababisha kioja kortini

Na RICHARD MUNGUTI

RAIA wa Pakistan alisababisha kicheko na wakati huo huo kuzua rabsha mahakamani Ijumaa alipomhoji kiongozi wa mashtaka sababu ya kupinga akiachiliwa dhamana ilhali Mbunge wa Embakasi Mashariki Paul Ongili almaarufu Babu Owino aliachiliwa na alikabiliwa na shtaka la kujaribu kumuua DJ.

Muhammad Adnan Tahir anayekabiliwa na shtaka la kupokea mali iliyo na thamani ya Sh10milioni akidai alikuwa na uwezo wa kuzilipia. Mshtakiwa alikana shtaka kisha akaomba aachiliwe kwa dhamana. Kiongozi wa mashtaka Bi Patience Bange alipinga ombi hilo akisema mshtakiwa yuko na pasipoti tatu na akiachiliwa atatoroka.

Baada ya kusikia mazugumzo ya Bi Bange mshtakiwa alijibu na kusema kwa masikitiko,”Mheshimiwa mbona kiongozi wa mashtaka anapinga nikiachiliwa ilhali Babu Owino aliyekabiliwa na shtaka la kujaribu kuua kisha akaachiliwa kwa dhamana.Alikuwa anatembea huru na alishtakiwa kujaribu kuua DJ.”

Bw Muhammad alimweleza hakimu mkazi R K Ondieki kwamba ameoa Mkenya na “kamwe hawezi toroka na kuacha rasilmali zake.” Mshtakiwa aliendelea kueleza hakimu mali anayoshtakiwa kupokea ni yake na kamwe hawezi kukaidi maagizo ya mahakama.

Bw Ondieki atatoa uamuzi ikiwa atamwachilia kwa dhamana mshtakiwa mnamo Feburuari 22,2022.

You can share this post!

Kibarua akana kuiba Vaseline

CHARLES WASONGA: ODM iridhike na urais, ikome kuzozania...

T L